Hasara Roho Lyrics by Darasa

Ah kama unataka kiki kwa pikipiki
Mara black mara white vipi
Kama unatikisa kibiriti
I play no game I’m sorry rafiki
Ukija kama upepo utapepea
Ukijifanya una mapepo tunakemea
Kama unataka mchezo kawashe runinga
Siku hizi hakuna mtu anataka ujinga
Ujanja wa nyani mjini utaingia kingi
Meli inaelea feri inazama shilingi
Haraka na harakati zako za pimbi
Unataka kucheza wewe na ushike filimbi
Binadamu angekua neja
Maneno yangeshutiki kama risasi
Vitu vingine vikienda
Havirudi reverse kama samaki
Hasara roho inachopenda tunasemaga pesa makaratasi
Hakuna wasiwasi tukaze mwendo ili tuende na wakati eh
Tuweke tuzo za wachukiaji
Bongo kuna watu wana vipaji
Utarusha madongo kwenye maji
Bora upige michongo utanipa midadi
Mara chenga mara no networki
Zigizaga vitu havieleweki
Life siku hizi imezidi kuwa complicate
Ukichanganya na mambo ya internet (jeraha)
Mwisho utatukana picha ukutani (jeraha)
Si atutafuti mchawi nani
Sasa chagua utajifungia chumbani
Au unatoka goma lipo uwanjani
Kushoto kulia juu chini kamatia
Mzigo wa abiria dereva dakia
Kichwa cha panzi alewe sifa kama pia
Situko serious we unatuactia eh
Binadamu angekua neja
Maneno yangeshutiki kama risasi
Vitu vingine vikienda
Havirudi reverse kama samaki
Hasara roho inachopenda tunasemaga pesa makaratasi
Hakuna wasiwasi tukaze mwendo ili tuende na wakati
(eh na wakati eh)
Utasema nakudisi
Ila mi mwenyewe unanimix
Mengine ni madalansi na sura ya machungwa utajua vipi
Kuji switch switch
Nusu viatu mtu fifty fifty
Hujafai hutaki chai moja haikai mbili haifai we wapi una fit eh (eh)


https://www.youtube.com/watch?v=G352NjZxbhs Here is the official Music video

Comments

Popular posts from this blog

Number One By Le Band and Suzziah Lyrics

Senzenina By King Kaka Lyrics

Sema Milele Lyrics by Gilad